Monday, 12 August 2013

ARUSHA UPDATE: MUUGUZI WA KCMC ANYONGWA HOTELINI, AFA




ARUSHA: (JAIZMELALEO)-Muuguzi wa Hospitali ya KCMC mjini Moshi aliyefahamika kwa jina la Renalda Nemes Minja ameuawa kwa kunyongwa na waya wa umeme Jijini Arusha imebainika.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjTEhSyk7qtzer_RC3COFpKZ5W5f3o0y98wuJUk1BM49Fe1S6NIF6xCy3a2UaQbjsv7Vn6DDJvjdG1cs37M-6e8NbB7fghvDArNtMaFz7lG5YQIGTxPkYLMWffoZcAa7r-ddeqGLZGWCe0X/s400/Police1.jpgDuru za Habari kutoka mjini Moshi siku ya Jumamosi (Agosti 10, 2013) mwaka huu zilisema Muuguzi huyo alitoka mjini Moshi na kuwaaga wenzake kwamba anakwenda kupata mapumziko ya mwishoni mwa juma jijini Arusha. 
Hata hivyo chanzo kingine kimedai kwamba muuguzi huyo mwenye umri wa miaka 32 alikuwa na tabia ya kutoka na wapenzi wengine nje ya mpenzi wake.
Pia ilikuwa ni tabia yake kupata mapumziko Jijini Arusha kila mwishoni mwa juma endapo hayuko katika zamu hospitalini hapo, kiliongeza chanzo hicho.
Hadi mauti yanamkuta alikuwa Jijini Arusha.
Jeshi la Polisi mkoa Arusha limesema mwili wa Marehemu ulikutwa katika Hoteli ya Home Suit iliyopo Mianzini Jijini Arusha.
Aidha Kaimu Kamanda wa Polisi Arusha, Japhat Lusingu amesema muuaji amefahamika kwa jina la Letare Lema (40) mkazi wa Moshi mkoani Kilimanjaro.
Lusingu amekitaja chanzo cha mauaji hayo kuw ani wivu wa mapoenzi ndio ulisababisha muuaji kufanya unyama huo.
Pia Kaimu Kamanda huyo amesema Muuaji amekamatwa na yupo mahabusu kwa mahojiano zaidi na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mount Meru. 

0 comments:

Post a Comment