Mwanamke mzee mwenye umri wa miaka 53
amejifungua watoto mapacha wa binti yake, baada ya madaktari kuthibitisha kuwa
bintiye hatoweza kubeba mimba.
UKISTAAJABU YA MUSA UTAYAONA YA FIRAUNI…
Suzie
Kozisek (53) mama mkazi wa Iowa nchini Marekani mwenye watoto wanne amejifungua
watoto wa bintiye aliyekuwa na matatizo ya via vya uzazi na Shinikizo la Damu.
Duru
za Habari kutoka jimboni humo maarufu kwa jina la American Heartland zinasema
mwanamke huyo mzee alitumika kwa kitaalamu “carrier” wa kubeba mayai ya binti
yake kupitia njia ya “Vitro Fertilization”.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa na Good Morning America imesema mwezi Juni, 2011 binti yake anayefahamika kwa jina la Ashley Larkin
alijifungua mtoto aliyempa jina la Harper.
Baada
ya kujifungua ikagundulika Larkin ana matatizo ya via vya uzazi licha ya mayai
ya uzazi “ovaries” kuwa mazima pia matatizo ya “Pulmonary Hypertension” ambayo
ingemzuia kuzaa tena.
Hivyo
walitokea wengi waliojitolea kuchukua mimba mingine ya binti huyo kutokana na
ukweli kwamba asingeweza kuzaa kwa njia za kawaida na hata kama angebeba
ujauzito angeweza kupoteza uhai wake.
Kozisek
wenye watoto wane walio na umri kati ya miaka 20 na 30 alipandikizwa mbegu za
kiume zilizokuwa tayari kwenye mayai ya Larkin na kisha kuwekwa kwenye Uterus
yake mwezi 2012.
Shirika
la Habari la ABC News linasema kazi ya kuyapandikiza mayai na manii ilifanyika
Okotoba mwaka 2010 katika Kiliniki moja iliyofahamika kwa jina la Mayo nchini
humo.
Mwanamke
huyo mzee alipandikizwa mimba amejifungua mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu.
Kozisek
ambaye ni Katibu Muhtasi wa taasisi moja mjini Iowa alikaririwa akisema kwa kipindi chote hadi anajifungua alikuwa
mwenye afya tele ambaye hakuweza kupatwa na lolote baya.
Kwa
upande wake Binti yake alisema watoto wake waliopewa majina ya Hallee na Hadlee
anaona ni Baraka pia ni muujiza.
Daktari
mmoja wa Kliniki ya Mayo aliyejitambulisha kwa jina la Jan Jensen ambaye ndiye aliyefanya
kazi ya uchavushaji huo na mtaalamu wa masuala ya Ujauzito kwa kina mama amesema
Larkin alipobeba mara ya kwanza hakuwa na tatizo lolote na kwamba alikuwa
mwenye afya njema kabisa.
Dk.
Jensen aliongeza kusema Kozisek umri wake haviendani na kuchukua ujauzito huo
hata kama ni kwa uchavushaji.
Daktari
huyo ameongeza kusema anamsifu Kozisek kwa ujasiri wa kumpenda bintiye na
watoto akiamini ni jambo la kushangaza lakini ndio lilivyo limetokea.
CHANZO: ABC News/Good Morning
America/YAHOO News.
0 comments:
Post a Comment