Wednesday, 7 August 2013

AMERICA NEWS: MTOTO WA MIAKA 6 AMSAIDIA RAFIKI YAKE MGONJWA




Jonah Pounazarian ni miongoni mwa watu 100 nchini Marekani wanaougua ugonjwa unaojulikana kwa jina la GSD-Glycogen Storage Disease Type 1B.
http://humanityrestored.com/wp-content/uploads/2013/02/chocolate-bar-book.jpg
Miaka ya 1980’s ugonjwa huo kwa walioupata walifariki wakiwa na umri wa miaka 2.
UKISTAAJABU YA MUSA UTAYAONA YA FIRAUNI…
Dylan Siegel ni mtoto mwenye umri wa miaka 6 ambaye ni rafiki wa ukweli wa Jonah.  Dylan anataka kumsaidia rafiki yake awe katika hali nzuri na kuandika kitabu cha matumaini ambacho kitawaingizia mamilioni ya dola kupata matibabu.
Dylan amekipa jina kitabu hicho kuwa ni “Chocolate Bar” ambacho kilichukua muda wa saa moja kukiandika na kukitafsiri.
Jina hilo ambalo kitabu hicho kimepewa limetokana na watoto wa kiume (wavulana) kulitumia nchini Marekani wanapotaka kuwasilisha ujumbe wao katika masuala ya kustaajabisha ama kuogofya.
http://bitchinsuburbia.com/wp-content/uploads/2012/11/Dylan_Jacob_final1.jpgMtoto Dylan aliwaambia wazazi wake David na Debra Siegel kumsaidia kukitoa katika machapisho ambayo yatasaidia kupata fedha amabzo zitatumika kumtibu rafiki yake.
Wazazi wake walitii na kutoa katika machapisho katika kichapishio(printer) cha kawaida nakala 200 ambazo waliziuza katika shule.
Baada ya kufanikisha hivyo Debra alikuwa na mataumaini kwamba watauza nakala walizotoa. La kustaajabisha ni pale walipoanza kuuza kitabu hicho ndani ya saa chache wakawa wamejikusanyia kiasi cha Dola 6000 (sawa na TZS 9,600,000/=).
Baba wa Dylan, David alisema kuwa waliamua kutoanakala kwa mara ya pilii na kuiweka katika FACEBOOK na baadaye katika mtandao . 
David aliongeza kusema  watu walianza kusikia na kukihitaji kitabu hicho na hivyo kufikia Malengo ya mtoto wao Dylan aliyowaomba wamsaidie ili rafiki yake aweze kupona.
Miezi 6 baadaye kitabu “CHOCOLATE BAR” kilikusanya kiasi cha dola 200,000 (sawa na TZS 320,000,000/=).
GSD ni ugonjwa amabao hushambulia sana Ini, na kwamba Mtoto Jonah hujikuta akishindia cornstarch kama chakula pekee ili kuendeleza uhai wake.
Lora Pournazarian alikaririwa akisema huwa wanachanganya na maji na kumnyesha ili kusababisha damu ya Jonah kuendelea kuwa na sukari.
Jonah aliruhusiwa kula vyakula vingine lakini kiwango cha sukari kimekukwa kikiangalia.
http://cdn-ugc.mamaslatinas.com/gen/constrain/500/500/80/2013/02/27/11/d4/p4/po306cctss.pngWazazi wa Jonah walisema tangu mtoto wao aanze kuugua wamejikuta wakijifunza kitu, kwamba ni kwa namna gani maisha ni tunzo ya tahamni sana kwa maisha ya mwanadamu kuliko chochote.
Mapacha Jonah na kaka yake Eli wanajisikia fahari kwa kitu ambacho rafiki yao Dylan amekifanya kwao kwa ajili ya kuokoa maisha ya Jonah.
Daktari Weinstein ambaye ni mtafiti wa magonjwa likiwemo GSD  amesema sio wote wanaolifahamu gonjwa hilo lakini pia akapigia nara kitabu cha CHOCOLATE BAR  kitachangisha fedha kwa ajili ya kuweka uelewa kuhusu GSD.
Daktari huyo amekiita kitabu hicho “DYLAN’S EFFORTS’’ (yaani Jitahada wa Dylan).
Jonah na Dylan kwa mara ya kwanza walikutana shuleni wakiwa na umri wa miaka 3 katika Chekechea moja nchini humo na mpaka sasa hawajaachana na kwamba urafiki wao utadumu.
CHANZO: BROKEN DAILY NEWS/HLNTV.com/TODAY.com

0 comments:

Post a Comment