Tuesday, 6 August 2013

Kujiuliza kwanini kunaweza kukusaidia kuelewa na kutatua tatizo.




Kujiuliza ‘’KWANINI’’ unapotafuta ufumbuzi wa tatizo ni njia moja wapo ya kukusaidia kutatua tatizo au kukusogeza karibu na chimbuko la tatizo. Utumiaji wa KWANINI umewasaidia watu wengi kujua chimbuko halisi la matatizo yao na kwa kujua hivyo wamekuwa wakitatua mambo mbalimbali na kufanikiwa.
Unapopatwa na tatizo ukijiuliza kwanini huzaa swali lingine la kwanini  hatimaye utasogea karibu na kujua ‘’Nini kilisababisha tatizo husika.”
Hebu tuangalie faida za kujuiliza swali hili kwanini.

  • Kujiuliza kwanini kutakusaidia kutambua kiini au mzizi wa tatizo. 
  • Kujiuliza kwanini ni rahisi kujifunza na kuelewa tatizo lako hatimaye kukusaidia kujua mbinu sahihi ya kutumia kutatua tatizo hilo.

Na sasa namna ya kutumia mbinu hii ya kutatua tatizo.
-Unapoendea kutatua tatizo anza kuangalia mwisho wa tatizo ambao ni matokeo ya tatizo lilipotokea kurudi nyuma kwa maana ya kuelekea mwanzo wa tatizo kwenye mzizi wa tatizo. Rudia kujiuliza ‘’KWANINI’’ ukiendelea kutafakari sababu mbalimbali za tatizo lako mpaka hatimaye ukaribie kiini cha tatizo.
-Ifuatayo ni mifano ya kuonyesha ni jinsi gani kujiuliza KWANINI kunasaidia kutatua matatizo mbalimbali.
1. Mfano wewe ni mfanyabaiara, unajiuliza kwanini wateja wako wanapungua siku hizi? Unagundua ni kwasababu hutoi huduma nzuri kwa wateja wako kama walivyotegemea kuhudumiwa. Baada ya kujua sababu ya tatizo unaamua kuboresha biashara yako kwa kuwajali wateja na kukua tena kibiashara.
 2. Mfano wewe ni mfanyakazi  ofisini,  unajiuliza kwanini hamkuweza kumaliza kazi ndani ya muda mliokubaliana? Unagundua kazi ilichukua muda mrefu kumaliza tofauti na mlivyotegemea. Mnaamua kuanzia sasa kazi zote za kiofisi ambazo zina uharaka na ni muhimu lazima zipangwe mapema na kukadiriwa uzito wake kiutendaji na kuzingatia muda ili kuepusha kuvunja makubaliano yenu.
 3. Mfano wewe ni mwanafunzi, unajiuliza kwanini haukufanya vile? Unagundua ni kwasababu haukupanga ratiba yako vizuri na kujua nini cha kufanya wakati huo. Baada ya kujua sababu unaamua kuwa kila kazi utajiwekea malengo na kufanya mambo yako kama inavyotakiwa.
 4. Mfano wewe ni mkulima, unajiuliza kwanini ulikadiria vibaya ukubwa wa kazi? Unagundua ni kwasababu ulifanya makadirio ya haraka ya eneo ulilotegemea kulima hivyo hukumaliza ndani ya muda uliopanga. Unaamua kazi zote zitakazofuata ni lazima ufanye makadirio sahihi ya namna utakavyofanya na kuzimaliza kwa wakati.

Mpendwa msomaji kuna njia nyingi sana za kutumia katika utatuzi wa matatizo, leo tumeona ni jinsi gani ''KIJUILIZA KWANINI'' kunasaidia kujua na kuelewa vizuri matatizo. Kujua mbinu zaidi endelea kusoma Life Skills Blog.
Kama una chochote cha kuongeza kuhusiana na mada hapo juu, tafadhali usisite kutoa maoni yako!

0 comments:

Post a Comment